Showing posts with label Accident Upcountry. Show all posts
Showing posts with label Accident Upcountry. Show all posts

Tuesday, September 22, 2009

Passanger Bus On Fire!

Above and below, the bus under fire
Passangers of this bus were lucky, they were all saved and nobody was hurt except the driver when this bus caught fire.


Thursday, August 27, 2009

Another Accident,8 killed 52 Injured!

Scanlink bus which overturned after the accident

8 people died in a road accident, 52 others have been injured in a road accident, which occurred yesterday morning at Maguha Village, Dumila in Kilosa District Morogoro region. The bus was heading for M, Scanlink, was travelling to Mwanza.
Amongst the dead are 4 women and 3 women and a girl aged 6 months named Kwimba Sengeti whose mother has been admitted at the hospital following injuries from the accident.
Some of the dead are yet to be identified and their bodies are at the Morogoro Mortuary.It has been said that the cause of the accident was a slippery road due to rain.
The driver of the bus is yet to be identified and the police in Morogoro continues with the investigation.Some of those injured expressed their despair that, after the accident they were robbed by villagers living near the area of the accident.
"Some of the villagers pretended to be good samaritans assisting the victims, but they robbed us of mobile phones and bags", they said.

Wednesday, August 26, 2009

Ajali Zaua Watatu Moro!

Watu watatu wamefariki dunia mkoani katika ajali mbili za barabarani zilizotokea mwishoni mwa wiki.
Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Thobias Andengenye, alisema kuwa ajali ya kwanza ilitokea Agosti 20 katika eneo la Kiegea wilayani kilosa barabara ya Morogoro-dodoma mkoani hapa.
Andengenye alisema katika ajali hiyo gari aina ya sprinter lililokuwa likitoka jijini Dar es salaam kuelekea Singida liliwagonga watembea kwa miguu na kusababisha vifo vyao. Aliwataja waliofariki kuwa Mwanaidi Husein(200 na Anath Daglas(2) wote wakazi wa kiegea wilayani kilosa, chanzo cha ajali bado hakijafahamika.
Katika ajali nyingine gari lisilofahamika lilimgonga mtembea kwa miguu Jumanne husein(40) mkazi wa Chamwino manispaa ya morogoro (Mwananchi).

Friday, August 7, 2009

10 Die, 35 Injured!

From ABBY NKUNGU in Singida.
TEN people died on the spot and 35 others were seriously injured, when a bus they were travelling in overturned at Sagara village on the Singida -Arusha road, about 55 kilometres from here. The accident occurred around noon and involved the bus christened 'Jordan', which was travelling from Moshi to Mwanza. Reports say the bus overturned after its driver lost control on a steep slope. The doctor in-charge of the Singida Regional Hospital, Dr Aubrey Mushi has since confirmed the deaths. However, he could not release names of the dead or the injured. An eyewitness said the bus had been speeding before it overturned. “It then rolled three times before it landed upside down,” said the witness, one of the Good Samaritans who rushed out in efforts to help the victims. The accident comes hardly three days since President Jakaya Kikwete called upon the Ministry of Home Affairs to review the Road Safety Act, to allow for sterner measures against reckless driving. About two weeks ago, another road accident claimed 28 lives after a bus from Nairobi to Dar es Salaam collided head on with a lorry in Korogwe, Tanga region. Last week, yet another accident left 12 people dead, when a lorry they were travelling in overturned in Babati.
Source: Daily News

Tuesday, July 28, 2009

Maiti wa Ajali ya Tanga Watambuliwa!

WAKATI Jeshi la Polisi nchini likitangaza majina ya abiria waliokufa na waliojeruhiwa katika ajali ya basi la Mohamed Trans lililogongana uso kwa uso na lori wilayani Korogwe, mkoani Tanga, serikali imetoa takwimu zinazoonyesha kukithiri kwa ajali mbaya za barabarani nchini.
Akizungumza jana kwenye eneo la tukio, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, James Kombe alisema kuwa watu waliothibitika kufariki kwenye ajali hiyo ni 28 na 14 kujeruhiwa. Hadi jana maiti 13 walikuwa wametambuliwa na miongoni ni ya mmoja wa madereva wa basi la Mohamed Trans, Joseph Kamitee.
Mwingine ni Ramadhani Kipsto, dereva wa lori lililohusika kwenye ajali hiyo linalojulikana kama Simba Track, ambalo lilikuwa linatoka Dar es Salaam kwenda Arusha.
Wengine ni raia wawili wa Marekani akiwamo Catheline Brooke Baxter mwenye paspoti namba 089355273 iliyotolewa New Orleans na Francis Kanyoike, raia wa Kenya. Wote walikuwa wamepanda basi hilo lililokuwa linakwenda Dar es Salaam likitokea Mwanza kupitia Nairobi, Kenya.
Kombe aliwataja maiti wengine kuwa ni Hassan Ramadhani (35) Julius Mollel (40), Mkadara Saidi Athumani (32), Ludovic Mselle (48), Ainaini Maro (53), Wisdom Mmasa (17) na Ramadhani Shaaban (30).
Vilevile, aliwataja Baraka Shaaban (21), Mohamed Saidi Cheka (Utingo wa Lori), Hagilori Utrikari (43) mwenye asili ya Kiasia, Neema Robert (24), Helen Jamhuri (37), Mbaruku David Kassanda (35), Daniel Owino (34) na Cathyrin Brooke (32).
Maiti wote wamehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo baada ya kubainika kuwa majokofu katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, hayafanyi kazi ipasavyo.
Alisema ajali hiyo ilitokea baada ya gurumu la mbele la basi hilo kupasuka na kwa vile lilikuwa katika mwendo mkali, dereva alishindwa kulidhibiti na kwenda kuliparamia lori hilo lililokuwa linakuja mbele.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Rashid Said alisema majeruhi wawili wa ajali hiyo, hali zao zilikuwa mbaya na ilibidi wasafirishwe hadi Dar es Salaam ili wachunguzwe na kutibiwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Majeruhi hao aliwataja kuwa ni Maria Kika, mkazi wa Moshi na Mary Erasnos ambapo wote wamepata majeraha vichwani. Hata hivyo, alisema majeruhi ambao wataendelea kupata matibabu hospitalini hapo ni Erasmos Mathias, Nelson Giatu na Lugano Martin (mmoja wa madereva wa basi).
Majeruhi wengine ni Ahmed Abdallah (22) wa Nairobi, Abdallah Ademi (22), Peter Nyakua (43), Mtunzi Selemani(32, Mary Erasmus (27), Hellen Alex (23), Jane Njeri (33), Jenipher Mushi (29), Nelson Gitau (40), Jimmy Massawe (32) na Ludovic Mcharo.
Wakati huo huo, serikali jana ilitoa tamko ikisema kuwa licha ya ajali hiyo, tayari watu 1,468 walikuwa wamekufa na wengine 8,373 kujeruhiwa katika ajali 10,168 za barabarani zilizotokea nchini katika kipindi cha Januari na Juni, mwaka huu.
Tamko hilo lililosainiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha na kusambazwa kwenye vyombo vya habari jana, licha ya kusikitishwa na kasi ya wimbi la ajali hizo, lilitaja hatua kadhaa ambazo serikali imekusudia kuzichukua.
Masha alithibitisha kuwa katika ajali ya juzi iliyotokea Korogwe mkoani Tanga watu 28 walipoteza maisha, 18 wakiwa wanaume na 10 wanawake.
Alibainisha kuwa waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni14, kati yao wanawake watano na tisa ni wanaume. Masha alilalamika kwamba, ajali hizo zimeendelea kutokea licha ya serikali kutoa taarifa, maelekezo ya mara kwa mara na elimu kwa umma.
Alisema uchunguzi wa polisi unaonyesha kuwa ajali nyingi zinatokana na madereva wazembe wanaoendesha magari bila kuzingatia sheria za barabarani, hasa mwendo kasi. Kwa upande wa mabasi ya abiria, Masha alisema: "Chanzo chake kikuu ni pamoja na mwendo kasi, ubovu wa magari, uzembe wa wenye magari kwa kutoyakagua mara kwa mara, ulevi na makosa mbalimbali ya kibinadamu."
Pamoja na usugu huo wa madereva kutobadilika, Masha alisema kuwa serikali haijakata tamaa na itaendelea kuimarisha doria katika barabara kuu, ukaguzi wa magari ili kuyazuia mabovu na kuielimisha jamii ili itoe taarifa polisi wanapogundua dereva anaendesha vibaya.
Hatua nyingine alizitaja kuwa ni kuendelea kuboresha sheria za usalama barabarani, kuhimiza elimu kwa madereva, kukagua na kuhakiki uhalali wa leseni na kuwabana wamiliki wa magari ili waajiri madereva waaminifu na wanaowajibika katika kazi zao. Katika tamko hilo, Masha alitoa pole kwa wote waliopatwa na msiba pamoja na majeruhi katika ajali hiyo.
Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jeneral Said Kalembo jana alizungumza na wananchi waliofika kwenye eneo la ajali hiyo na kuwatahadharisha kuwa wanaposafiri dereva akiendesha basi kwa mwendo wa kasi, watoe taarifa polisi ili waweze kudhibitiwa.
"Nawapa mkono wa pole ndugu wa waliokufa katika ajali hii, ni janga kubwa limetukuta Tanga, lakini nawaomba abiria mkiwa katika magari yanayoendeshwa kwa kasi toeni taarifa polisi," alisema Kalembo.
Naye Kombe alieleza kukerwa na mtindo wa baadhi ya madereva wa magari ya abiria kuendesha kwa kasi wakati wakijua wamebeba roho za watu. Mmoja wa majeruhi aliyejitambulisha kwa jina la Erasmus Mathias alisema ajali hiyo ilitokea baada ya tairi la la basi upande wa kushoto kupasuka na baadaye kulivaa roli na kisha magari yote yakaanguka.
"Dereva wa basi kama angekuwa amekwenda mwendo wa kawaida yasingetokea maafa kama haya," alisema Nasoro Juma, mkazi wa Kijiji cha Kwakombo.
Taken from: www.mwananchi.co.tz

Monday, July 27, 2009

Ajali Ya Mohamed Trans Yaua 30!

ZAIDI ya watu 30 wamefariki dunia baada ya basi walilokuwa wakisafiria la Mohammed Trans, kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam kupitia Nairobi nchini Kenya, kupata ajali wilayani Korogwe mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti la Mwananchi kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Erasto Sima, zinasema chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa gurudumu moja la basi hilo na kugongana uso kwa uso na gari la mizigo aina ya Scania, lililokuwa likitoka Dar es Salaam kwenda Arusha.
Mpaka gazeti linakwenda mtamboni ni majeruhi 13, ndio waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Korogwe, Magunga, mkoani Tanga na katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo, iliwekwa taa ya kandili kutokana na kukosekana kwa umeme ili shughuli za kuweka miili ya marehemu hao ziendelee .
Habari zaidi zilisema ajali hiyo ilitokea katika eneo la Kwa Kombo wilayani Korogwe, majira ya saa moja jioni jana.
Sima alisema jitihada za kutoa maiti nyingine ambazo zinadaiwa kuwa zimekandamizwa na basi hilo, zilionekana kuwa ngumu kiasi cha kuagiza winchi kutoka mjini Tanga, lisaidie kuliinua basi hilo ili maiti zilizokandamizwa ziweze kupatikana.
Hata hivyo, mkuu huyo wa wilaya alisema hadi muda huo kulikuwa na maiti 27 zilizokwisha patikana, wanaume 21 na wanawake sita.
Wakati huohuo, mtu mmoja amefariki dunia katika ajali iliyotokea maeneo ya Wami mkoani Tanga baada ya gari la Kampuni ya Airbus lililokuwa likisafiri kwenda Dar es Salaam jana kugongana na lori.

Taken from: www.mwananchi.co.tz

Sunday, June 28, 2009

Sheikh Suleiman Gorogosi Dies! Another Victim of Road Accidents!

The Acting Chief Sheikh of Tanzania Suleiman Gorogosi was killed on Saturday in a motor traffic accident in Lindi Region. It is being reported that the vehicle he was traveling in suffered a tyre bust and rolled over.May Allah Rest his Soul In Eternal Peace, Amen!

Source: Faustine's Baraza

Thursday, June 25, 2009

Ajali Yaua 7 na Kujeruhi 41 Mbeya!

WATU saba wamefariki dunia na wengine 41 kujeruhiwa vibaya baada ya Lori aina Fuso lenye namba za usajili T855 ACJ kugongwa kwa nyuma na lori aina ya SCANIA lenye namba za usajili T 463 kupinduka korongoni katika mlima wa Iwambi kuelekea Mbalizi mkoani Mbeya. Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa lori aina ya Fuso lilibeba watu waliokuwa wakitokea mazishini ambalo lilikuwa mbele ya SCANIA lililokuwa katika mwendo wa kasi hivyo dereva wa gari hilo alishindwa kulimudu ndipo tela la gari lake lilipoligongalori na kusababisha kuanguka korongoni.
Photo Source: Food for thought blog

Friday, June 12, 2009

Maiti 3 Zatambuliwa...Ni Ajali ya Hajees!

Miili ya watu watatu kati ya watu sita waliofariki katika ajali ya gari iliyotokea katika kijiji cha Mtumba kilometa 20 kutoka dodoma imetambulika.
Ajali hiyo ilitokea juzi eneo la mtumba manispaa ya dodoma ambapo watu 6 walipoteza maisha huku wengine 37 wakijeruhiwa wakiwamo 18 waliolazwa katika hospitali ya mkoa wa dodoma wakiendelea na amatibabu.
Mkuuwa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa dododma Salum Msangi alisema maiti zilizohifadhiwa katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma zimetambuliwa kwa kuangalia vitambulisho vilivyokutwa katika mifuko ya marehemu hao.
Msangi aliwataja waliotambuliwa kuwa ni Dk. Shabani Kibwana wa Hospitali ya Mtakatifu Gasper iliyopo itigi wilayani Manyoni, askari wa jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ) kutoka makao Makuu dar es salaam mwenye namaba MT 69547 PTE Mohamed Salum na Jackson Alex.
Alisema jeshi la polisi linaendelea kumsaka dereva wa basi hilo aliyetoroka muda mfupi baada ya ajali na kwamba uchunguzi wa awaliunaonyesha kwamba dereva alikuwa kwenye mwendo kasi kutokana na basi hilo kuserere pembeni umbali war obo kilometa baada ya ajali hiyo kutokea.
Basi lililopata ajali ni la kampuni ya Hajees.
Source: www.mwananchi.co.tz
blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker