Tuesday, January 27, 2009

AJALI ZAENDELEA KUUA

Wiki iliyopita, ajali ilyotokea mkoa wa Arusha iliteketeza maisha ya wananchi za idi ya 20 kufuatia ajali kati ya lori na basi la abiria aina ya Coaster. kwa weli inasikitisha sana kuona maisha ya watanzania kama hawa wanateketea.

Ni katika kipindi hicho hicho ajali iliteketeza watu wanne baada ya gari kuwafuata walipokuwa wanatembea kwa miguu maeneo ya mwananyamala. Tunachotaka kuonyesha hapa ni kwamba, kiukweli ajali zinaua watanzania wengi amabao kwa njia moja au nyingine wanategemewa sana na taifa hili.

Tunawapa pole ndugu wa wale waliopoteza maisha-Mr.Bobos Class Team.

Friday, January 23, 2009

KIGAMBONI WAKOMBOLEWA

Wakazi wa Kigamboni jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita walifarijika sana kupatiwa kivuko cha MV Magogoni. Hatua hiyo ilifuatia kilio cha miaka mingi cha wakazi wa eneo hilo wakilalamika kwamba wanaweza kupoteza maisha kutokana na ajali ambayo ingeweza kutokea kutokana na ubovu wa kivuko kilichokuwepo. Kwa hatua hiyo tunaipongeza serikali kwani imeepusha maafa.

Sunday, January 18, 2009

BARAZA NALO LAGUSWA.

Kile kinachoonekana kuwagusa wadau mbalimbali wa nyanja ya usafiri sasa kimeligusa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nchi Kavu na Majini(SCCC), nacho ni ongezeko la ajali zinazoteketeza maisha ya watanzania wengi kwa sasa hivi. Mwenyekiti wa Baraza hilo Bwana Gilliard Ngewe katika taarifa yake ya wiki hii alisema kwamba “…ili kuondokana na matatizo ya upandishaji wa nauli kiholela, alitoa wito kwa taasisi zote zinazohusika na sekta ya usafiri kuanza kuandaa mchakato wa kuendesha usafiri kwa njia ya makampuni. Alifaamisha kuwa kampeni hiyo itaenda sambamba na kutoa elimu kwa madereva kuhakikisha madreva wanapimwa kiasi cha pombe walichokunywa wakiwa wanaendesha gari na kwamba dereva yeyote atakayekamatwa anaendesha gari akiwa amekunywa pombe atanyang’anywa ufunguo na hataruhusiwa kuendesha kwa siku hiyo.lengo likiwa ni kupunguza ajali za barabrani zinazotokea mara kwa mara na kuua watu wengi”.
Inatia moyo sana kuona kwamba kila mdau katika nyanja ya usafiri anaguswa na tatizo hili la vifo visivyo vya lazima vinavyosababishwa kwa kiasi kikubwa na uzembe wa madereva kwa kuendesha wakiwa wamelewa au kutozingatia sheria za barabarani na matokeo yake ndio hayo tunayoyaona. Wengi wanaguswa wanaposikia kwamba ajali imeua makumi ya watu, lakini husahau baada ya muda mfupi tu. Ni jukumu la kila mdau na hata mwananchi wa kawaida kupinga vifo visivyo vya lazima vinavyotokana na uzembe wa madereva.(Kwa msaada wa gazeti la Mwanachi na vyanzo vingine)

Saturday, January 17, 2009

KAMPUNI YA BIA(TBL) YACHANGIA ELIMU

Ikiwa ni jitihada za watu binafsi na makampuni kuiunga mkono serikali katika vita vyake dhidi ya ajali nchini, Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) ilichangia kiasi cha shilingi Milioni 2.2 kusaidia kuchapisha vipeperushi vya kuelimisha jamii na madereva kuhusu sheria na kanuni za usalama barabarani.
Mr. Bobos Class Team tunaipongeza kampuni hiyo, kwani mchango wake ukitumika vema utaokoa maisha ya watu na mali zao kwa kuwakinga na ajali mbalimbali.
Msaada huo uliwakilishwa kwa Mrakibu Msaidizi wa Polisi(ASP) Joseph Mwakabonga na Bwana Maneno Mbegu ambaye ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL).

MOTOR VEHICLE ACCIDENTS


''Motor vehicle accidents'', also known as ''Auto Accident or road traffic accidents (RTA’s)'', are a frequent and cause of property damage, personal injury, and death. Motor vehicle accidents can result from a collision with a building, tree, telephone pole, animal, human, or other motor vehicle. The legal ramifications of a motor vehicle accident are proportionate to the severity of incident. Parties involved in an Automobile Accident are required to stop at the scene and exchange insurance and identification information, or call the police. Failing to stop after an accident is a serious offense known as a “hit and run.” Individuals involved in a motor vehicle accident may face criminal and/or civil liability. The state does not usually prosecute. However, if there is evidence of gross negligence, severe injury, or death, the state may find that legal action is necessary. In these cases, the offender may be charged with driving under the influence of drugs or alcohol, assault with a deadly weapon, manslaughter, or even murder. The resulting penalties vary greatly, ranging from incarceration to the death penalty. Civil liabilities following a serious Auto Accident include personal injury lawsuits, fines, and the suspension or revocation of one’s license.
Visit
Lawyer Central to find out more.

AFRIKA INAONGOZA KWA AJALI?

Ni hali ya kusikitisha kuona kwamba idadi ya watu wanaopoteza maisha kutokana na ajali Afrika, inazidi kuongezeka siku hadi siku. Hali ambayo imelishtua hata Shirika la Afya Duniani (WHO). Maneno yafuatayo hapa chini ni ushahidi tosha wa haya ninayosema kulingana na utafiti uliofanywa na BBC mwaka jana na kufuatiliwa na wadau mbalimbali ndani na nje ya Afrika.
Inasema kwamba:
‘’Trauma rates in Africa are among the highest in the world. According to the World Health Organization, each year there are more than 200 000 road traffic deaths in Africa and perhaps 20 to 30 times as many people seriously injured. And trauma in Africa is definitely getting hotter, with injury rates predicted to increase by around 80% by 2020’’.

Hizi si takwimu za kufurahia, ni takwimu ambazo zinaonyesha kama hatua za kudhibiti hali hii hazitachukuliwa, hali itaendelea kuwa mbaya na watu wengi watapoteza maisha kutokana na ajali. Watu 200,000 kupoteza maisha sio kitu kidogo au cha kuangalia tu na kuacha kiendelee kuchukua maisha ya watanzania.
Swali lakujiuliza ni kwamba, “Je, katika hiyo idadi ya vifo 200,000 vya ajali ni vingapi vimetokea Tanzania?” kwa jinsi idadi ya ajali inavyoongezeka, ni dhahiri kwamba mchango watanzania katika idadi hiyo ni mkubwa sana kuliko mtarajio ya wengi. Katika wiki hii, ajali ya Basi la Tashrif iliyotokea Mji wa Hale Mkoani Tanga, imechukua maisha ya watanzania wasiopungua 28 na wengine 24 walijeruhiwa vibaya. Na tangu mwaka huu wa 2009 uanze idadi ya watanzania waliopoteza maisha katika ajali mbalimbali ni zaidi ya 70? Je, tunaridhika na hali hii na kukaa kimya?
Profesa Ian Robertson (Professor of Epidemiology and Population Health) anasema kwamba:
‘’One pointed out that doctors needed to do 30 trauma laparotomies to make the grade in trauma surgery. This can take three years in the north but only three months in Johannesburg’’.
Kwamba kwa daktari kutoka uingereza anatakiwa kufanya operesheni za tumbo (Laparatomy) kwa majeruhi wa ajali 30 kwa wagonjwa wa ajali, na akiwa Uingereza au nchi yoyote ya Ulaya itachukua miaka mitatu kupata idadi hiyo ya wagonjwa. Lakini kwa mshangao, ukiwa Afrika katika jiji la Johannesburg unapata idadi hiyo ndani ya miezi mitatu. Na Ninathubutu kusema Tanzania idadi kama hiyo itapatikana ndani ya miezi miwili kulingana na takwimu za ajali zinavyokwenda kwa sasa hivi.
Wadau wote katika fani ya masuala ya ajali, tunatakiwa kufunga mikanda ili kudhibiti hali hii inayoonekana kutishia maisha ya watanzania wengi.
Binafsi ninapongeza hatua zilizochukuliwa na SUMATRA (Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini) kwa kuyafungia kutoa huduma mabsi ya makapuni ya Sumry, Air Buffalo,na Zuberi kutokana na kutokidhi viwango vya biashara ya usafirishaji Abiria na kuhatarisha usalama wa maisha na mali zao.
Kwa kufanya hivyo nina imani kwamba, si tu maisha ya watanzania yataokolewa bali pia uharibifu wa mali zao na miundo mbinu utadhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Aluta Continua!

Wednesday, January 14, 2009

HUDUMA YA KWANZA INAOKOA MAISHA

Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa jili ya ugonjwa au majeraha. Kwa kawaida hutolewa na na mtu yeyote ambaye hajasomea tiba mpaka msaada wa kitalaam unapofika.Baadhi ya magonjwa yanaweza yasihitaji msaada zaidi wa matibabu baada ya kupata msaada wa huduma ya kwanza. Kwa kawaida huduma ya kwanza huwa ni hatua rahisi ambazo mtu anaweza kufunzwa na kutumia vifaa rahisi.
Huduma ya kwanza inaweza kutolewa kwa wanyama waliojeruhiwa pia, lakini inahusisha zaidi binadamu.
Swali tunalopaswa kuulizana ni kwamba, je ni maisha ya watanzania wangapi ambayo yamepotea kwa kuwa watanzania wengi hawajui kutoa huduma ya wkwanz? Ni mara ngapi tumeonea watu wakiwasaidia majeruhi wa ajali mbalimbali lakini katika kufanya hivyo wakiwazishia maumivu zaidi au hata kusababisha vifo vyao? Inasikitisha.
Taarifa hii inafuatilia uchunguzi uliofanywa na wadau wa ‘‘Mr. Bobos Class’’ na kugundua kwamba, watanzania wengi hawajui kutoa huduma ya kwanza hasa hasa kizazi kipya ambacho kimekumbana na mapungufu ya taaluma hiyo mashuleni.
Kwa waliosoma miaka ya nyuma wamebainisha kwamba wao walijifunza hudma ya kwanza kwa njia mbili; kwanza, walifundishwa mashuleni kama sehemu ya masomo yao, pili, wale waliokuwa maskauti walijifunza katika mafunzo ya uskauti.
Ni dhahiri kwamba watanzania wengi wamepoteza maisha yao katika ajali mbalimbali kwa kuwa wale waliokuwa karibu yao walishindwa kuwapa huduma ya kwanza.
Hivyo mjadala unafunguliwa wadau wote wanaombwa kuchangia nini kifanyike ili kuhakikisha kwamba watanzania kwa ujumla wao wanajua kutoa huduma ya kwanza.

Monday, January 12, 2009

MOI YALAZA 5, NA MMOJA AFARIKI

Taarifa tulizozipata leo wakati tukisherehekea sikukuu ya Mapinduzi ya zanzibar ni kwamba, Taasisi yaTiba ya Mifupa MOI imepokea wagonjwa wa ajali mbalimbali wapatao watano. Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa uhusiano Mwandamizi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) Bw. Jumaa almasi.
Majina ya waliopata ajali ni kama ifuatavyo;Sudi Magenge ambaye ana umri wa miaka 40, alipokelewa MOI akitokea Mkuranga baada ya kupata ajali na kuumia kichwa na kuvunjika mkono wa kushoto. Mwingine ni Abdallah Mohamed Abdallah mwenye umri 23,ambaye alipata majeraha ya kichwa. Pia Albert John aliyepokelewa kutoka hospitali ya Mwananyamala akiwa aamevunjika mfupa wa paja. Mwisho ni Abasi abdallah Juma mwenye miaka 26, alipokelewa MOI kutoka hospitali ya Amana akiwa amepata majeraha sehemu mbalimbali za mwili na kuvunjia mfupa wa mkono karibu na kiganja(Ulna),mfupa wa mguu chini ya goti(Tibia na Fibula), mfupa wa mguu sehemu ya paja(femur) na kuumia kichwa (Mild head injury).
Kwa mujibu wa Bw. Almasi, wagonjwa wote hao wanaendelea vema baada ya kupatiwa Tiba, lakini kwa bahati Mbaya Abdallah Mohamed Abdallah alifariki dunia pamoja na jitihada kubwa zilizofanywa na madaktari kuokoa maisha yake.
NI MASIKITIKO MAKUBWA KWA KIJANA MWENYE UMRI MDOGO KAMA HUYU ABDALLAH MOHAMED ABDALLAH(23) KUPOTEZA MAISHA WAKATI NDIO KWANZA ALIKUWA KATIKA UMRI WA KUANZA KUTEGEMEWA. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI NA MAJEERUHI WALIOBAKIA WAPATE AHUENI YA HARAKA. AMIN.
HAYA YOTE NI MADHARA YA AJALI.
Wanaopata ajali hapa nchini ni wengi, na wengi wao hupata hata ulemavu na kusababisha maisha kuwa magumu sana kwao na wale wanaowategemea. ni wachache sana ambao wanajua ni hatua gani za kuchukua baada ya kupata ajali kama hizo-hasa ajali za gari. Kwa kiasi kikubwa wengi wa wale waliopata ajali walikuwa abiria katika vyombo mbalimbali vya usafiri hususan magari. na imebainika kwamba, mara nyingi ajali hizo hutokea kutokana na uzembe wa dereva, aidha anakwenda mwendokasi, anaendesha amelewa au hata kuendesha kwa kutozingatia madhara kwa abiria wake.
Japo ataadhibiwa kwa mujibu wa sheria za nchi, lakini je anajua ni watu wangapi amewaharibia maisha kutokana na uzembe wake?
Kwa hiyo blog hii pia ina lengo la kuwaonyesha hao madereva madhara waliyowaachia abiria na familia zao. Kwa mfano mtu aliyevunjika kiuno na kupooza kuanzia kiunoni hadi miguuni ni wazi kwamba hatoweza tena kufanya kazi za kujikimu yeye na familia yake. kwa maana hiyo familia nzima inakuwa imeathirika kwa ujumla.
hivyo blog hii itawaletea mifano halisi ya watu ambao wameathirika kutokana na ajali mbalimbali.
blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker