Saturday, February 14, 2009

AGONGWA NA KUFA PAPO HAPO!

Mwendesha pikipiki ,yenye namba za usajili T 831 AVN, Rajab Said (31) amefariki baada ya kugongwa na gari katika barabara ya Mbande jijini. Abiria aliyekuwa amebebwa katika pikipki hiyo aliyejulikana kwa jina la Mohamed Said alijeruhiwa vibaya sana. Gari lililosababisha nii aina ya Toyota Corolla yenye namba za usajili T956 ADQ lililokuwa likiendeshwa na Ramadhani Kapata(32) akitokea Chamazi kwenda Mbagala. Hiyo ni kwa mujibu wa Taarifa ya Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Emannuel Kandihabi.
katika tukio jingine, Kamanda wa Mkoa wa kipolisi Ilala,Faustine Shilagile, alitoa taarifa kwamba Kulwa Lucas au Lugame mkazi wa mtoni sabasaba alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari akijaribu kuvuka barabara. Ajali ilitokea jana majira ya saa 1.30 usiku katika barabara ya Nyerere katika njia panda ya Jet.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker