Sunday, February 22, 2009

Maoni ya Wadau Kuhusu Ongezeko la Ajali Nchini.

Ifuatayo ni taarifa niliyoikuta katika blogu ya Damija(http:www.damijablogspot.com) iliyopostiwa tarehe 17 January 2009 na nikaona ni muhimu wadau wengine pia wapate ladha. Karibuni.
AJALI ZA BARABARANI ZINATUMALIZIA WAPENDWA WETU BONGO....Ujumbe toka kwa da'Janeth Jesse.
Napenda kuleta dukuduku langu kwa wadau wote wa blog yetu ya jamii ili tulijadili ktk kujenga kuhusu AJALI ZA BARABARANI BONGO,jamani kwakweli tumechoka watu wanateketea imefikia steji sasa na tuseme ENOUGH IS ENOUGH sasa na sisi,haijatimia hata week1 tangia basi la kampuni ya TASHRIFF liwafyeke abiria zaidi ya nusu waliokuwa wakisafiri (30)na wengine 29 kulazwa ktk hospital za Muheza teule na Bombo Tanga,huu ni msiba mkubwa sana UHAI NI KITU CHA THAMANI NAFUU MTU AKUIBIE HELA AU MADINI KULIKO AKUTOE ROHO YAKO.Basi la kampuni hiihii wadau mkumbuke lilishawahi kupoteza maisha ya abiria (78) lilipofunikwa na maji meneo ya kibanda Muheza, Tanga.KITU GANI kifanyike wadau kuepuka vifo vya kizembe vya namna hii?dereva kaua kakimbia ni mhuni anakabidhiwa chombo kilichobeba roho za watu,kwa uzoefu wangu wa kuishi bongo miaka mingi naamini karibia nusu ya waendesha magari daresalaam mjini hawana leseni na nusu ya waendesha vyombo wanaendesha wamelewa,ni kawaida kuwakuta watu wamepaki magari yao bar wanakunywa pombe kisha wanaendesha,jamani jamani tunauana jama.HILI JESHI LA POLISI KITENGO CHA TRAFFIC utawakuta wote wana vitambi kwa rushwa na kutafutia watu leseni kwa njia za mazabe.JK MAISHA BORA NI PAMOJA NA SHERIA KALI ZA BARABARANI KWANI ZINAHUSU UHAI AMBAO NI KITU CHA THAMANI KULIKO CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)....MunguIibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika. Mdau wa Kwasemgaya safarini DENMARK mara1
Posted by Mija Shija Sayi at
10:15 PM
1 comments:
Koero Mkundi said...
Hii misemo ya kiswahili wakati mwingine huwa inanitatiza,eti ajali haina kinga, hivi kweli huu msemo bado una exist?Na je bado unafundishwa huko mashuleni? kama bado unatumika na unafundishwa huko mashuleni, basi juhudi za serikali kutoa elimu ya usalama barabarani ni kazi bure.Utafundishaje elimu ya usalama barabarani wakati tunambiwa ajali haina kinga?Nadhani umefika wakati wa hizi methali, misemo na nahau zetu kuchunguzwa kama zinaenda na wakati maana nyingine zinatufundisha uzembe. Naomba kutoa hoja.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker