Saturday, February 21, 2009

MADHARA YA UDEREVA USIO MAKINI!


Kila kukicha, vyombo vya habari vinaripoti juu ya ajali mbalimbali ambazo hupoteza maisha na mali. Pichani ni mwathirika wa ajali ambaye amepoteza kiungo muhimu katika maisha yake, mguu. Hivyo maisha yake hayatakuwa kama ilivyokuwa mwanzoni kabla ya ajali.

Akieleza tukio la ajali hiyo, kijana anayeonekana pichani (jina limehifadhiwa)alisema kwamba ilikuwa majira ya saa moja usiku huko Mkuranga, akitoka matembezini, gari lililokuwa ikienda kwa kasi sana lilipasuka gurudumu la mbele na hivyo gari liliyumbayumba na kumfuata yeye akiwa pembeni mwa barabara, likamgonga na halikusimama tena likakimbia.Hakujua kilichotekea kwani alipoteza fahamu. Wasamaria wema walimbeba na kumpeleka hospitali ya Mkuranga na hatimaye akapewa rufaa hadi Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ambapo wataalam waligundua kwamba mguu umeharibika kabisa na hivyo ikabidi ukatwe chini ya goti.

kutokana na uzembe wa dreva huyo, kijana anayeonekana pichani amepata ulemavu wa kudumu.

Mr Bobos Class tunampa pole kwa matatizo yaliyompata.ushauri tunaompa ni kwamba kupoteza kiungo sio mwisho wa maisha.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker