Sunday, February 22, 2009

TAFADHALI FUNGA MKANDA KUOKOA MAISHA




Katika picha zinazoonekana katika habari hii, ni gari (pick-up)iliyogongana na trekta uso kwa uso. Dereva alikuwa ni mwanamke mwenye umri wa miaka 30 ambaye alikufa papo hapo. Pembeni yake Katika alikuwa abiria mwenyeumri wa miaka 28, aliyejeruhiwa vibaya sana na hata jinsi ya kumtoa ilikuwa ni kazi nzito.


Kiti cha nyuma kulikuwa na watoto watatu ambao wote hawakuwa wamefunga mikanda ya kiti. Mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka 3, alitupwa chini ya kiti akabanwa na kufa papo hapo. Mtoto mwingine mwenye umri wa miaka 12 alikufa papo hapo baaday kutupwa tupwa ndani ya gari kwa ajili ya kutofunga mkanda, na mtoto wa mwisho mwenye umri wa miaka 15 aliokolewa na kupelekwa hopitali akiwa mahututi.


Dereva wa trekta hakuumia hata kidogo. Inasemekana dereva wa pick-up alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi bila kujali hali ya unyevunyevu iliyokuwepo barabarani.


Tuna imani kwamba, iwapo waliokuwepo ndani ya gari wangefunga mikanda kiwango cha madhara kisingefikia hapo(Picha kwa hisani ya www.cars-accident.com).


Somo: Ni muhimu kufunga mikanda tuwapo katika vyombo vya usafiri kuokoa maisha na mali.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker