Wednesday, February 25, 2009

Kwa Mtindo Huu....!!!



Kwa mtindo huu nadhani jitihada za kudhibiti ajali hapa nchini itakuwa ni sawa na "Kupigia Mbuzi Gitaa" kwa maana ya kwamba ajali zitaendelea na watu watapoteza maisha kama tunavyoshuhudia. Picha hii ilipigwa kutoka katika treni ya Reli ya Kati maeneo ya Mkoa wa Singida. Cha kwanza, basi limejaa mpaka watu wamekaa juu sehemu ya mizigo; Cha pili, basi likuwa linaenda kwa mwendo wa kasi ili kushindana na treni bila kujali kwamba barabara linapopita basi si nzuri ina mashimo na mengine ni makubwa sana. Bahati kutokana na umbali namba z usajili za basi hilo hazikupatikana, lakini wenyeji wa huko wakiona rangi ya basi watajua ni basi la kampuni gani.
Wadau, nafikiri kazi ya kupambana na ajali ni kubwa na nzito kuliko inavyoonekana, lakini kwa jitihada za pamoja nina imani tutashinda na hatimaye kuokoa maisha na mali(Picha na Hamisi Bilali-DSM)

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker