Monday, February 16, 2009

WAATHIRIKA AJALI YA ARUSHA KUDAI FIDIA

Waathirika wa ajali iliyotokea hivi karibuni katika barabara kuu ya Arusha-Moshi, katika daraja la Mto Nduruma wilayani Arumeru, wameshauriwa kuandaa taratibu za kudai fidia kutoka katika bima ili waweze kulipwa haki zao.
Ushauri huo umetolewa mwishoni mwa wiki mjini Arusha, na Katibu wa Baraza la Huduma za Usafirishaji Nchi Kavu Bw. Oscar Kikoyo alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Usimamizi na Ushauri wa Huduma za Usafirishaji Mkoa wa Arusha, kuhusu utaratibu wa waathirika wa ajali hiyo kuwasilisha madai yao ili walipwe fidia.
Amesema kuwa kwa mujibu wa sheria mbalimbali zinazotawala sekta ya usafirishaji nchini, ikitokea ajali ni lazima wenye chombo cha usafiri, pamoja ba bima kumlipa mwathirika wa ajali ikiwa ni pamoja na waliopoteza maisha(Taarifa hii imeandikwa na Magesa Magesa wa gazeti la majira 16 Februari, 2009).
Hoja yangu: Ni jambo la kutia moyo kuona kwamba kuna vyombo ambavyo vipo tayari kutoa ushauri na kuwasaidia walioathirika katika ajali mbalimbali kudai haki kwanii wengi wa waathirika hupoteza haki zao kwa kutojua au wanapoona zoezi zima la kudai fidia linakuwa ni mlolongo mrefu.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker