Sunday, February 1, 2009

MAISHA ZAIDI YATEKETEA!

Wiki inayoishia leo zimetokea ajali ambazo zimeteketeza maisha ya wananchi kadha na kuwaacha wengi wakiwa majeruhi.
kwa kujibu wa gazeti la "Habari Leo" la tarehe 31 Januari 2009, lilikuwa na kichwa kisemacho "Ajali zaua watu 15", watu 15 walikufa katika ajali zilizohusisha magari na treni katika mikoa ya Daresalaam na Morogoro huku zikiacha majeruhi zaidi ya 20.
Katika ajali hizo mbili iliyotokea Dar es salaam watu 9 walikufa papo hapo na wengine 10 kujeruhiwa na ajali ilitokea maeneo ya Jet Club, Kipawa barabara ya Nyerere, wakati Morogoro watu 6 walikufa papo hapo na wengine 10 kujeruhiwa katika ajali ya treni ya Kampuni ya Reli Tanzania(TRL).
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, inaonekana kwamba ajali zote zilisababishwa na uzembe wa madereva. Dreva wa dalala lenye namba za usajili T700 Toyota Hiace "kipanya" lililoua watu 9, aliligonga lori lenye namba za usajili T452 ACP ambalo lilikuwa limepinduka. Inasemekana "kipanya" kilikuwa kinafanya safari za usiku tu kutokana na leseni yake kumaliza muda wake.
Kwa kweli inasikitisha kuona kwamba, wakati jitihada za makusudi zinafanywa na wadau mbalimbali ili kuokoa maisha na mali za wanaopata ajali, bado kuna wachache ambao wanafanya uzembe wa makusudi na kurudisha nyuma jitihahada zote hizo.
Mr. Bobos Class tunaamini kwamba sheria itachukua mkondo wake na wale wote watakaobainika kuwa na makosa ya uzembe watachukuliwa hatua kali za kisheria.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker