Sunday, February 22, 2009

Ajali Ya Basi la Wachezaji Nigeria!

Basi la timu hiyo liligongana uso kwa uso na basi jingine la abiria. Ado Umar kiongozi wa timu hiyo alifariki hapo hapo na mchezaji Abdullahi Sabiu alifariki jumamosi hospitali.Ajali hiyo pia ilipoteza maisha ya watu wengine watano wa basi la abiria.Wachezaji kadhaa wa timu hiyo walijeruhiwa kutokana na ajali hiyo na bado wanaendelea na matibabu katika hospitali moja katika mji wa Gombe.Afisa wa chama cha soka cha Nigeria (NPL)Tunji Babalola alisema kwamba timu hiyo ilikuwa ikisafiri kuelekea mji wa Gombe kucheza na timu ya Wikki Tourist katika mechi ya ligi ya Nigeria.Ajali hiyo mbaya imekuja mwezi mmoja baada ya timu nyingine ya daraja la chini Jimeta United kupoteza wachezaji wake 17 na viongozi wa timu baada ya basi lao kupata ajali wakati wakielekea Abuja kwenye mechi ya ligi. (Na Mohamed Kindindi -Nifahamishe.com)

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker