Monday, February 16, 2009

DAKTARI WA MIFUGO AFA AJALINI.

Habari iliyopatikana katika gazeti la Majira la leo inaripoti kwamba, gari lililokuwa likiendeshwa na mhandisi wa shirika la Ugavi wa Umeme nchini(TANESCO) tawi la Moshi, mkoani Kilimanjaro, limepata ajali na kumuua Daktari wa Mifugo, Bw. Amani Tete anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 40-45.
kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Lucas Ng'hoboko alisema marehemu marehemu ni daktari wa mifugo Machame, wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na gari iliyopata ajali ni Toyota Chaser yenye namba za usajili T132 ATE. alisema ajali ilitokea eneo la mnadani Weruweru katika barabara kuu ya moshi Arusha.
Hoja yetu: Ajali za barabarani zina madhara makubwa kama inayoonekana katika ajali hii kwamba mtaalamu ambaye Taifa linamhitaji ameshapoteza maisha na kuacha pengo si kwa ndugu na jama, sehemu anayofanyia kazi bali ni kwa Taifa kwa ujumla. TUENDESHE KWA UANGALIFU KUZUIA AJALI.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker