Thursday, May 14, 2009

Kubeba Watoto Katika Baiskeli!


Mara nyingi nimekutana na waendesha baiskeli wakiwa wamewabeba watoto katika kiti cha nyuma cha baiskeli. Leo asubuhi saa 12.30 nimemuona huyu bwana katika picha(bofya picha) akiwa amembeba mtoto(angalia mshale) ambaye alikuwa anaonekana aidha amechoka au ana usingizi wa kuamshwa asubuhi sana kuwahi shule.Ninachoona mimi, huyu mtoto mikono yake haina nguvu kama ya mtu mzima, njia anayopita ni ina mashimo mashimo na inarusha kiasi kwamba huyu mtoto anaweza kuachia na kudondoka. Naomba tunapoona hilo tukemee ili kunusuru maisha ya watoto kama huyu.


No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker