Friday, April 24, 2009

Kutoka MOI!Shattered Dreams?


Kijana Salum Saleh baada ya kukatwa miguu yote
Kijana Salum Saleh(19) amelazwa taasisi ya Tiba ya Mifupa na Magonjwa ya Ajali Muhimbili (MOI) kufuatia kupata ajali mbaya iliyosababisha yeye kupoteza miguu yote miwili baada ya madaktari kuona uwepo wake unahatarisha maisha ya Salum.
Anasema kwamba,yeye ni mchuuzi wa nguo mikononi, na siku hiyo alipanda daladala ili kutoka Mwenge kwenda Tazara. Dereva wa gari hilo alikuwa anaendesha mwendo kasi na abiria wakaanza kumfokea ili apunguze. Yeye alikuwa miongoni mwa abiria waliokuwa wanakemea mwendo wa dereva huyo na alimfuata na kumwambia.Hii ilileta mtafaruku kidogo na ndipo wakati anashuka makondata walimsukuma, gari likampanda miguuni na kumsukumia katika mfereji wa maji machafu kiasi cha kumpa infection ambayo baada ya masaa machache miguu ilibadilika rangi na kuanza kutoa harufu mbaya sana.
Ili kuokoa maisha yake, ilionekana ni vema miguu yote iondolewe. Kijana Salum(pichana)amepoteza miguu yote,imebaki sehemu ndogo tu ya paja. Salum amekuwa mlemavu ghafla, ndoto za maisha yake zimeisha badilika na anakata tamaa ya kuishi.

(Salum Saleh,19,lost both legs following motor traffic accident. He was pushed by the bus conductor of a passenger bus he was in, following a misunderstanding between him and the bus operators. Having fallen down the bus tyres ran over his legs and pushed him in a drainage with contaminated water.His open wounds were infected instantly, which led to severe gangrene. Then,both limbs had to be amputated up to his thighs to save his life. Salum is desparate, lost hope and his life dreams are gone! )

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker