
Katika jitihada za kuhakikisha feeder roads zinafanyiwa matengenezo na kutumiwa na madereva ili kupunguza ajali,nimekuwa nikizifuatilia na kuzitumia hizi feeder roads mbalimbali. Kuna hii ya kutokea OilCom mwembechai kupitia Grand Hotel, DDC Magomeni Kondoa hadi Kawawa Road, narudia tena kwamba hii ni barabara muhimu kama itafanyiwa matengenezo. Kuna eneo korofi lililopo mbele ya DDC MAgomeni Kondoa ambalo majiu hutama mwaka mzima(Pichani).Mvua ikinyesha linakuwa dimbwi kubwa sana ambalo si rahisi kwa magari madogo kupita. Wahusika watuambie, kuna mipango gani!
No comments:
Post a Comment