Thursday, April 30, 2009

Mabomu Yajeruhi na Kuua!(Explosions at Armoury)

Watu walipochanganyikiwa na milipuko ya mabomu


Wauguzi wa hospitali ya Temeke wakiwashusha majeruhi MOI

Majeruhi akiwa chini ya uangalizi wa madaktari


Mmoja wa majeruhi aliumia kama hivi,na mwingine alipoteza mguu kabisa
Mtoto wa miaka saba ambaye hakutambulika jina lake hadi leo alipoweza kuongea na kusema kwamba anaitwa Khadija Zomboko. Anasema watu walipokuwa wanakimbia, walimkanyaga na kumvunja mkono!


Madaktari na maafisa wa MOI wakijaribu kupata maelezo kutoka kwa mmoja wa watoto waliofikishwa hapo.

Gari za wagonjwa kutoka kila kona ya Dar zilibeba majeruhi

Majeruhi wakishushwa MOI, palikuwa hapatoshi!


Wauguzi wa MOI wakimpatia msaada mmoja wa majeruhi



Kibaka chini ya ulinzi, "ati kufa kufaana, leo utashaa!"

Kibaka aliyejaribu kuiba wakati wa milipuko mbaroni


Masalia ya bomu lililolipuka

Moja ya nyumba zilizoathirika
Moshi mzito baada ya bomu kulipuka
Kaazi kweli kweli, wingu zito!
Wingu na moto! (Picha na Hamisi Bilali)

Kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ajali(MOI) taarifa inasema kwamba majeruhi waliofikishwa hapo ni 26,kati ya hao, wawili wamelazwa ICU, 14 wamelazwa,9 walipata matibabu na kuruhusiwa kwenda nyumbani na mmoja alipata matibabu na kupelekwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuwa alikuwa ni mja mzito, hivyo ataonana na madaktari bingwa wa kinamama.


Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano mwandamizi wa MOI Bw. Jumaa Almasi, walioumia sana ni Zulfa Hamisi ambaye amekatika mguu kutokana na mlipuko na Juma Sobo ambaye aliumia kichwani na kupoteza meno kadhaa.


Wakati huohuo, Rais wa Jakaya Kikwete akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi, Inspekta Jenerali wa Polisi, Waziri wa Afya Prof Mwakyusa,ametembelea MOI na kuwapa pole majeruhi waliolazwa katika Taasisi hiyo.


Kiongozi mwingine wa kitaifa aliyefika MOI ni Makamu wa Rais, Dr. Ali Mohamed Shein aliyefika kuwapa pole majeruhi pia.
(Rais Kikwete akiwa MOI ICU. Source: Michuzi Blog)



(More than 100 people have been injured following explosions at Dar es salaam Armoury. The bomb exploded from fourr out of 11 armouries at the camp of the Pople's Defence Force (TPDF) caused panic and paralysed activities for the whole day).

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker