



Mmoja wa majeruhi aliumia kama hivi,na mwingine alipoteza mguu kabisa










Masalia ya bomu lililolipuka





Kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ajali(MOI) taarifa inasema kwamba majeruhi waliofikishwa hapo ni 26,kati ya hao, wawili wamelazwa ICU, 14 wamelazwa,9 walipata matibabu na kuruhusiwa kwenda nyumbani na mmoja alipata matibabu na kupelekwa hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuwa alikuwa ni mja mzito, hivyo ataonana na madaktari bingwa wa kinamama.
Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano mwandamizi wa MOI Bw. Jumaa Almasi, walioumia sana ni Zulfa Hamisi ambaye amekatika mguu kutokana na mlipuko na Juma Sobo ambaye aliumia kichwani na kupoteza meno kadhaa.
Wakati huohuo, Rais wa Jakaya Kikwete akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi, Inspekta Jenerali wa Polisi, Waziri wa Afya Prof Mwakyusa,ametembelea MOI na kuwapa pole majeruhi waliolazwa katika Taasisi hiyo.
Kiongozi mwingine wa kitaifa aliyefika MOI ni Makamu wa Rais, Dr. Ali Mohamed Shein aliyefika kuwapa pole majeruhi pia.
(Rais Kikwete akiwa MOI ICU. Source: Michuzi Blog)(More than 100 people have been injured following explosions at Dar es salaam Armoury. The bomb exploded from fourr out of 11 armouries at the camp of the Pople's Defence Force (TPDF) caused panic and paralysed activities for the whole day).
No comments:
Post a Comment