Friday, March 20, 2009

Ajali Nyingine Pwani Yaua Saba!

Wakati majina ya watu 10 waliofariki kwenye ajali ya gari la abiria mkoani mbeya wakitajwa majina, ajali nyingine imetokea wilayani Rufiji na kuua watu 7, ikijeruhi wengine 20.
Jana Mwananchi iliripoti kuwa watu 20 wanahofiwa kufa katika ajali hiyo iliyotokea Barabara ya Tunduma kwenye maeneo ya Mbembera, njia panda ya JKT Itende, na eneo la Iyunga, lakini jana Mkuu wa Wialaya ya Mbeya, Leonidas Gama alisema ni watu 10 tu waliofariki kwenye ajali hiyo na si 20 kama mashuhuda walivyosema jana.
Katika ajali ya iliyotokea Mloka wilayani Rufiji, watu 7 walipoteza maisha na wengine 20 kujeruhiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka.
Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 8 mchana ikihusisha garilenye namba za usajili T 674 ADY mali ya kampuni ya Morning Star ambalo lilikuwa linatokea jijini Dar es salaam kwenda Mloka (Na julieth Ngarabali Mwananchi 20-3-09).

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker