
Mwingine ni Bwana Robert Masawe ambaye ameelezea tukio hilo kwamba, alikuwa anasubiri gari katika pembeni kabisa mwa barabara, daladala liliacha njia na kumfuata alipo na kumgonga. Robert aliteguka bega.
Mwisho ni Arumela Mwapalala(15) mkazi wa kimara alikuwa ana vuka barabara gari likamgonga ambapo alipata jeraha kubwa katika kidevu na kupoteza jino moja.alipata matibabu na kuruhusiwa kwenda nyumbani.
Afisa Uhusiano wa MOI Bwana Jumaa Almasi alisema kwamba, wagonjwa walifikishwa MOI na kupatiwa matibabu. Robert Masawe na Arumala waliruhusiwa , na Aisha alilazwa.
No comments:
Post a Comment