Wednesday, March 25, 2009

Wanne Wafa Ajali ya Gari, Pikipiki!

Watu wanne wamekufa na mmoja kujeruhiwa baada ya magari na pikipiki waliyokuwa wakisafiria kugongana katika barabara kuu ya Morogoro-Dar es salaam eneo la Nane Nane mjini hapa.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Ibrahim Mwamakula, alisema ajali ya kwanza ilitokea machi 21,mwaka huu saa 9.30 alasiri.
Kamanda Mwamakula alisema ajali hiyo ilihusisha basi la abiria lenye namba za usajili T 381 AXT aina ya FAU, mali ya Kampuni ya Tonda Express lililokuwa likitokea Njombe kuelekea jijini Dar es salaam. Alisema Basi hilo lilikuwa likiendeshwa na majid mohamed(46) liligongana na gari ndogo aina ya Toyota Corolla yenye namba T 666 AKJ ikiendeshwa na Sweetbert Kamugisha(28).
Wakati huo huo, mwendesha pikipiki na abiria wake wamepoteza maisha baada ya kugongwa na gari eneo hilo la Nane Nane.
Kamanda Mwamakula Alisema pikipiki iliyohusika katika ajali hiyo haikuwa na usajili ambapo iligongw na Toyota Corolla yenye namba T292 AET iliyokuwa ikendeshwa na Erick komba(26)(Nipashe).

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker