Monday, March 30, 2009

Sumatra ytakiwa Kuchukua Hatua Temeke!

Wakazi wa Temeke Mwisho jijini Dar es salaam wameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) kuzichukulia hatua kali za kisheria daladala zinazogoma kutumia kituo kipya cha Temeke Mwisho.
Wakizungumza na mwananchi, wakazi hao walisea tangu kituo hicho kikamilike ujenzi wake mwaka jana, bado hakijaanza kutumika kutokana na madereva wa daladala kugoma kukitumia kwa mdai kuwa hakina abiria.
Walisema ili kuhakikisha kituo hicho kinatumika na kuondoa ussumbufu wa kutembea mpaka Tandika ambako daladala hizo zinapaki, ni vyema Sumatra ikasaidia katika kuhakikisha kituo hicho kinatumika.
Kwa upande wao madereva wa daladala zinazotakiwa kutumia kituo hicho walisema itakuwa vigumu kwao kutumia kituo hicho kwa madai kuwa hakina abiria tofauti na kituo cha Tandika ambacho wanakitumia hivi sasa.
Kituo hicho cha Temeke Mwisho ambacho ujenzi wake uligharimu zaidi ya Sh. 70 milioni, kilitakiwa kuanza kutumika kuanzia Februari 2 mwaka huu kutokana na agizo la kikao cha baraza la madiwani mwisho mwa mwezi Januari(Mwananchi) .

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker