Tuesday, March 24, 2009

HALI YA BARABARA MBALIMBALI USIKU WA LEO(23-03-2009)

Hali ya barabara mbalimbali za jiji haikuwa shwari usiku wa leo. Kulikuwa na ajali eneo la Mkwajuni iliyohusisha garo ndogo na basi la Tanzania Road Haulage. Sikuweza kufahamu mara moja kama kulikuwa na majeruhi au la, lakini kilichoonekana ni msongamano mkubwa wa magari uliosababisha na ajali hiyo. Magari ya kuelekea magomeni na yale ya kuelekea morroco yalikuwa yanatembea taratibu sana.
Katika tukio jingine, kulikuwa na msongamano mrefu maeneo ya Kimara kutokana na magari kupunguza mwendo katika matuta ya barabarni, hivyo daladala zilikuwa zinapita pembeni mwa barabara kwa kasi sana hatimaye daladala moja linalofanya safari zake kutoka Ubungo kwenda Msata yenye namba za usajili T860 ATQ ilikuwa inaenda kwa kasi sana kuelekea Mbezi. Ilipofika kimara stop over, ilimgonga mama aliyekuwa na mtoto wake wakitembea pembeni mwa barabara. Baada ya kumgonga ilimpakia huyo mama ndani na kuondoka nae.
Sijui walimpeleka wapi!

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker