Thursday, March 26, 2009

Amwagwa na Pick-Up na kufariki!

Alikuwa akidaka kofia yake iliyopeperushwa na upepo.
Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Muteseka mugusi 32, amefariki dunia baada ya kudondoka toka kwenye gari akiwa kwenye harakati za kudaka kofia yake iliyopeperushwa na upepo.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa mwanza, Jamal Rwamboh, amesema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 11:00 jioni huko kwenye barabara ya Mriti Wilayani Ukerewe.
Amesema mtu huyo ambaye ni mkazi wa nakamwe Ukerewe alidondoka toka kwenye gari lenye namba za usajili T 316 ARR aina ya Nissan Pick-Up, lililokuwa likiendeshwa na dereva Maingu malima,25(Alasiri).

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker