Wednesday, March 18, 2009

MWENDESHA PIKIPIKI ANUSURIKA!

Katika kile kinachoonekana kuwa mwendelezo wa vitendo vya kiharamia dhidi wa waendesha pikipiki wanaobebaba abiria maarufu kama 'boda boda au mchubuko', juzi usiku alinusurika kuuawa na watu wasiojulikana. Wakisimulia mkasa huo, baadhi ya waendesha pikipiki wa eneo la mbezi kwa Musuguri wanasema kwamba, mwenzao alikodishwa na kijana amabaye hawamfahamu na alitaka kupelekwa eneo la 'Kwa Chale' kupitia njia ya Bwaloni. Wasema alimuelekeza huko lakini walipofika alidai amsogeze mbele zaidi. Na mwendesha pikipiki alishtuka na kujiandaa lakini walipofika mbele kidogo ya hapo kwa Chale, walijitokeza vijana wawili waliokuwa wamekaa pande zote mbili za barabara na kuinua waya ambao ulimkaba dereva wa pikipiki na kuanguka.
Lakini kwa kuwa ilikuwa majira ya saa moja usiku ambapo wapita njia walikuwa wengi, kijana huyo alipiga kelele na wasamaria wema walipojitokeza kiasi cha kuwafanya wezi hao wakimbie na kutokea gizani.

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker