Thursday, March 19, 2009

WATU 20 WAHOFIWA KUFA AJALINI MBEYA.
Zaidi ya watu 20 wanahofiwa kufa katika ajali ya barabarani baada ya lori la mizigo kugonga magari sita ikiwamo daladala katika eneo la Mbembela, lilopo Nzovwe, jijini Mbeya. Walioshuhudia tukio hilo walisema wamewaona watu wengi wakiwa wameumia vibaya baada ya lori hilo lililokuwa likienda kwa mwendo kasi likiyumbayumba na kisha likaligonga basi hilo aina ya Hiace.
Baada ya kuligonga gari hilo lililigonga gari jingine dogo lililokuwa umbali wa mita 10 kutoka katika basi hilo na kisha likaligonga gari jingine aina ya Landcruiser ambalo mbele yake kulikuwa na magari mengine mawili. Baada ya kugonga magari yote hayo moto ulilipuka(gazeti la Mwananchi 19-03-09).

No comments:

Post a Comment

blogarama - the blog directory
Directory of News Blogs
This blog gives information about accidents-vehicles,motorcycles,bycycles etc,also highlights the suffering of those involved in various accidents. It gives counselling to the accidents victims and information as to where they can get assistance be it legal or humanitarian.
Health blogs
eXTReMe Tracker